Style Pundits Everywhere Is a Free Daily blog that delivers the latest must see photos about hottest fashion trends with the twist of spicy pop culture gossip. Organize your wardrobe today.
Friday, August 10, 2007
Hili ni vazi la wapi tena?
Huyo ni Victoria Beckham akienda kuhudhuria party mahali.
I DIDN'T KNOW LINGERIE TURNS OUT TO BE EVENING WEAR.ALL YOU HAVE TO DO IS GET YOUR CORSET AND THROW ON SOME MIN COAT....DONE! BUT WITH THOSE HIGH HEELS.......YOU REAL ARE..... "PRETTY WOMAN"
Thursday, August 9, 2007
Miaka 50 ya kuzaliwa na midomo ya miaka 10
Tuesday, August 7, 2007
Flavor Flav is always ontime
Flavor Flav kama anavyojulikana na washabiki wake alikua ni mmoja wa wanamuziki wa kundi la Public Enemy lililovuma miaka ya themanini kama sio tisini mwanzoni.Jamaa huyu anayejulikana kama PIMP(mtu anayetumia wanawake kutengeneza hela) na mwenye signature ya kuvaa saa shingoni kama unavyoona kwenye picha,alijizolea washabiki wengi aliporudi katika television akiwa na kipindi cha kutafuta mwanamke wa kuishi nae.Hapo nyuma hao ni baadhi ya mabinti waliokua wanamgombania.Flavor Flava alipata binti ambaye yupo nae baada ya kujaribisha kipindi hicho cha TV kilichojulikana kama Flavor of Love mara mbili kilichokuwa kinarushwa katika station ya VH1 nchini Marekani.Hivi sasa anarudi ulingoni na mapishi.
DON'T WORRY FLAV, I WILL BE ONTIME EVEN IF I DON'T HANG A WALL CLOCK ON MY NECK.
Monday, August 6, 2007
Pale binti yako anapokuwa mpinzani
Wakati sakata la kuwania urahisi nchini marekani likiwa linapamba moto kati ya vyama viwili maarufu nchini hapa,siasa imeingia ndani ya nyumba ya mmojawapo wa wagombea madaraka hayo ya juu kabisa duniani anayeitwa Rudy Giuliani.Mzee Giuliani ambaye alikua mayor wa mji wa NewYork na mgombea urahisi aliye mstari wa mbele kwa wapinzani wake wa chama cha Republican ameshitushwa na habari za bintie ambaye kaamua kujiunga na kambi ya ugombea urahisi ya Baraka Obama.Kumbuka Baraka ni mweusi wa chama cha Upinzani cha Democrat na ana asili ya kenya anaungwa mkono na binti huyo ambaye kaamua kusaliti baba yake.Habari hizo zilizopatika katika website ya myspace.com ilionyesha picha za binti huyo akiwa na rafiki zake na wakimuunga mkono Mr Obama.Mzee Giuliani alipoulizwa kutoa maoni yake alisema kwa kifupi anafurahi kitu chochote mtoto wake anachofanya.
PROUD PAPA
Diddy anavinjari na mtoto wa kiingereza
Mwanamuziki/ mfanyabiashara maarufu nchini marekani P Diddy anafanya mpango wa kupumzika katika boat lake na mtoto wa kiingereza ambaye ni mcheza sinema hapa marekani Sienna Miller.Kulikua na maongezi ya chini chini kwa muda mrefu kuhusu uhusiano wa Diddy na Miller ambao ulipekea Diddy kutengana na mama watoto wake Kim P. Mwanamke huyo ambaye kamzalia watoto mapacha Diddy aliamua kuondoka zake baada ya kuona boyfriend wake anahangaika na wazungu.Sasa hatuna habari rasmi za romance kati ya watu hao wawili lakini uwezekano ni mkubwa maana wote wawili ni mabachela wa kutupwa.
WE HEARD YOUR STORIES DIDDY,IS IT TRUE?
Subscribe to:
Posts (Atom)