Wednesday, September 19, 2007

Wazee wa Macharanga!?


Kanye West aliungana na Diddy, Jay-Z na producer LA Reid katika sherehe ya kuadhimisha miaka 50 ya kuzaliwa kwa gazeti la GQ iliyofanyika jumanne(jana) Newyork.

Tuesday, September 18, 2007

Rosie amtolea nje Oprah


Kuna usemi nchini Marekani kuwa Oprah akikuita haukatai,lakini safari hii Oprah kakumbana na kukataliwa pale alipomwalika mtangazaji Rosie Odonnell katika kipindi chake ambapo alitaka wazungumzie kuhusu kitabu kipya cha Rosie kinaitwa "Celebrity Detox".Rosie anayejulikana kwa kukosoa watu na hasa wale wanaojulikana pamoja na kuropoka mambo mengi bila mpangilio, alimtumia ujumbe Oprah akimueleza hataweza kuhudhuria mwaliko labda siku nyingine.Bahati mbaya Oprah anakualika mara moja tu.
DEAL WITH IT BIG O